Friday, 5 August 2022

MVUTO WA KIBATALI

         MVUTO WA KIBATALI
     Kibatali  ni hatari sana kwenye mambo ya kuvuta mvuto. Inaingia katika mambo mengi sana kwenye mapenzi biashara kitu kilichopotea na vinginevyo vingi.
      Sasa leo nitaelezea mambo ya mapenzi na biashara twende sawa kama wewe umeangaika sana kumrudisha mke au mume umeangaika sana kumtuliza mweza wako lakini wapi sasa tafuta
kibatali na Utambi wake kama utakuwa umemchota mwenza wako mchanga wa unyayo wake, una nyuzi za nguo na kucha nywele utawek katika iko kibatali kama utakuwa hauna hivyo vitu andika
majina yake katik karatasi vitu unavyotaka ukimaliza fushia udi wako tia humo katika kibatali.
       Weka na dawa inaitwa Mvuto Mlipu Mchekea Itinginya Itetema Mwamba Ngoma.
Kananamba Makusanya Mpendwa Pendwa.
Mlangamia na Mliliwa weka mafuta ya taa yakutosha kila siku utawasha Asubuhi kwa manuizi yako unayo yataka kisha acha kibatali kikiwaka mpaka kizime nakupa tu dondoo utasemaπŸ‘‡πŸ‘‡
       "Fulani bin fulan kama moyo wako ulizima juu yangu mimi sasa leo nauwasha uniwaze mimi
nakulipua nakuita
mawazo yako fikira zako uniwaze mimi fulani bin fulani nakuvuta kwa nguvu ya Upepo, Udongo Moto, Maji akili yako yote hisisikie la kuambiwa na mtu yoyote yule".

     Mafuta yakiisha jioni utatia utawasha tena fanya hivyo siku saba atakuja mbio mbio uyo utamuonea huruma.


       KWENYE  BIASHARA  

  fagia hapo eneo lako la biashara upate mchanga wa hapo na mchanga wa njia zinazo ingia hapo katika biashara yako weka katika kibatali utachanganya na dawa hizi Mkulingu

Italigula Pangamanati Mkubwa Singelo
Mweunge Chababila utaweka mafuta yako ya taa na upukuchulie udi rose tumia kuwasha kwa manuizi ya Kuvuta wateja Wallah huto lala njaa hata mara moja.

WhatsApp
https://chat.whatsapp.com/E0YucVBI9X41qbIDBzux3f

Friday, 18 February 2022

ASALAM ALEYKUM ,YULE BINGWA WA TIBA ASILI AFRIKA MASHARIKI NA KATI MAALIM MAMBIKHI
                 πŸ“Œni Mganga wa Jadi anae tibu kupitia Miti Shamba na Kisomo, kama vile kwa yule alie achwa Mke, Mume, au Mchumba 
Maalim Mambikhi πŸ“Œ               atakurudishia kwa haraka sana Mvuto wa Biashara au Mapenzi, Mvuto Kazini na kupandishwa Cheo, Kumvuta aliekuwa mbali Mke,au Mume, Mchumba au Ndugu, Kuondoa Jini Mahaba,na Ndoto mbaya, Kumuona mbaya wako na Mgoni wako Kumkamata Mwizi wako kwenye Kioo cha Uganga.
  Maalim Mambikhi pia anaweka Zindiko la Mwili, Nyumba, Vyombo vya Usafiri, na Mashamba, kwa wale wanaosumbuliwa chango la uzazi mimba kuhalibika tatizo la Tezi,Maumivu chini ya Kitovu, Ngiri, Busha, Ganzi Mwilini, Miguu kuwaka Moto muone Maalim Mambikhi atakusaidia.
          MPUTA Ni dawa ya limbwata kwa Mke, au Mume,au Mchumba,na kumfanya akusikilize kwa kila unacho mwambia pia Pete ya bahati yenye kuambatana na Nyota ya Mwanadamu,kuzuia na  kutoa Chuma Ulete na mengineyo HUDUMA UTAIPATA POPOTE ULIPO DUNIANI 
WHATSAPP 
https://chat.whatsapp.com/C0GZ4Dtgow0Ges8ZEBM64n

Thursday, 17 February 2022

JIFUNZE TIBA ASILIA HAPAπŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡.

https://youtu.be/f8HZ2mZ6V3g Husipitwe na madarasa yanayoendelea Youtube. Kuwa wakwanza kupata Madarasa ya Maalim Dr.Mambikhi kwa Kulike na Kusubscribe Page ya

Wednesday, 16 February 2022

NYOTA ZENU LEO JUMATANO TAREHE 16/2/2022

         NDOO ( Jan 20- February 19)
Wiki hii inaonekana umekuwa mzito na Umesitasita  kwa muda mrefu kufanya maamuzi. Usiogope jitoe muhanga iwapo unataka kufaulu hasa katika mambo yako.

         SAMAKI ( February 20- March 20)
Utahitaji ushauri mzuri ili kuweka mambo yako sawa. Kutimia kwa mipango yako uliyonayo kunategeme wewe utajihusisha na mambo ya aina gani 

               PUNDA ( March 20-April 20)
Leo  imekuwa vigumu kwako kufanya maamuzi kuhusiana na mambo Fulani na utajikuta uko  njia panda itakayokutenganisha na mambo mengi. amua cha kufanya katika kufikia malengo yako unayoyataka.

                NGOMBE( April 21- May 20)
Umekuwa ukisumbuliwa na mikosi na matatizo sasa kwa muda mrefu na leo ndio hasa wakati hasa wa kuyashughulikia hayo matatizo yako na kuyamaliza. 

                MAPACHAMay 21- Juni 20)
Leo  uwe na hisani kwa kila mtu na jitolee kutoa msaada, tabia  hiyo itawafanya watu wakuthamini , ikiwezekamna   mara kwa mara toa msaada kama unavyotoa kwa wengine na wakija wasaidie wala usichoke

                  KAA ( Juni 21- Julai 22)
Leo badilika na  jiweke mbali na marafiki wabaya iwapo utataka kufaulu katika maisha yako. umekuwa ukitumia vibaya fedha zako kiasi cha kushindwa kutekeleza baadhi ya mambo yako ambayo umejipangia wewe mwenyewe, Acha hiyo tabia 

             SIMBA (Julai 22-Agosti 22)
Matatizo mengi ambayo yaliyokuandama yalikuwa yanatokana na mikosi  kwa upande wako, Tafuta njia ya kuondoa husda hiyo au nuksi hizo kabla hazijakuletea madhara kwa sehemu kubwa kwako, 

            MASHUKE  (Agosti 23-Sep 23)
Ondoa khofu. Nyota yako itakuletea mambo makubwa  na mengi sana katika maisha yako. Yakitokea hayo yakubali tu hatimaye utamakinika na utaona faida ya mabadiliko hayo. 

              MIZANI  ( Sep 23-Oktoba 23)
Leo  tafuta ufumbuzi au utatuzi wa shida zako zinazokukabili. Jiepushe na marafiki wasio na  tija kwako. Leo Unahitaji utulivu wa hali ya juu katika kutekeleza majukumu yako yanayokukabili.

                   NGE (Oktoba 23-Nov 22)
Leo ni  Jumatano nzuri sana kwako hasa katika kubuni mbinu na Mipango ya maisha yako  ya baadae, yaweke pembeni mambo ambayo unayaona hayana maana na simamia kile ambacho unakiamini

               MSHALE (Nov 22- Desemba 21)
Leo  tumia Jitihada binafsi kujielekeza kwa mambo mema unaweza kufanikiwa. Utakutana na mgeni na atakutaka muwe marafiki, mkubalie kwa sababu utapata faida kubwa kwa hilo hasa kwa wiki inayokuja. 

                MBUZI ( Desemba 21- Jan 20)
Siku ya leo Kuna bahati kubwa sana ipo upande wako ,watu wengi watakuchangamkia na watakuwa tayari kukusaidia kuyashughulikia matatizo yako yanayokukabili

Wednesday, 2 February 2022

SIRI YA HERUFI YA MWANZO YA JINA LAKO KINYOTA

SIRI YA HERUFI YA MWANZO YA JINA LAKO KINYOTA

          Je Unajua Siri ya herufi ya mwanzo ya jina lako?. Soma hapa utaweza kuelewa Tabia zako au tabia za rafiki au mpenzi wako.

                           HERUFI A
        Mwenye jina linaloanziana na herufi A ni mtu anayependa mambo makubwa, anajiamini na mwenye uwezo wa kutimiza malengo yake. Ni mtu mwenye tahadhari, mchangamfu na mpenda matukio. Anapenda Kuheshimiwa, anapenda Mamlaka, na ana kiburi, na hasira. Herufi A inawakilisha Nyota ya Punda.
                       HERUFI B
          Mwenye jina linaloanziana na herufi B ni mtu, mkarimu, muaminifu, na hupenda kazi. Ni Jasiri, shujaa na mkatili katika vita au pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake. Herufi B inawakilisha Nyota ya Ngombe,
                       HERUFI C
         Mwenye jina linaloanziana na herufi C ni mtu wa kukubadilika badilika, mshindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda. Ni watu wa wabunifu na wanaopenda mawasiliano Herufi C inawakilisha Nyota ya Mapacha,
                        HERUFI D
           Mwenye jina linaloanziana na herufi D ni mtu anayependa usawa, Biashara. Ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi. Ni jeuri na wenye msimamo. Herufi C inawakilisha Nyota ya Kaa,
                      HERUFI E
         Mwenye jina linaloanzia na herufi E ni mtu mwenye roho nzuri ,yenye mapenzi na huruma. mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Kinyume na hivyo atakuwa ni mtu asiotegemewa na kigeugeu. Herufi E inawakilisha Nyota ya Simba,

                      HERUFI F
        Mwenye jina linaloanzia na herufi F ni mtu mwenye mapenzi,huruma , roho nzuri na ana uwezo wa kuwafariji watu. Ni mtetezi wa watu na mwenye huzuni lakini ni mzito wa kufanya maamuzi. Herufi F inawakilisha Nyota ya Mashuke,
                       HERUFI G
         Mwenye jina linaloanzia na herufi G ni mtu mwenye mwenye imani ya kidini na nguvu za kiroho. Ana kipaji cha kubuni na uwezo wa kutatua matatizo ya watu. ni mtu mwenye hisia kali,msomi, mpweke na mkaidi wa kukubali ushauri wa kutoka kwa watu. Herufi G inawakilisha Nyota ya Mizani,
                       HERUFI H
        Mwenye jina linaloanzia na herufi H ni mtu mwenye ubunifu na nguvu katika biashara, hupata faida kubwa kutokana na jitihada na bidii zake. ni mwenye mawazo mengi, mchoyo na mbinafsi. Herufi H inawakilisha Nyota ya Nge,
                      HERUFI I
        Mwenye jina linaloanzia na herufi I ni mtu mwenye kupenda sheria, ana huruma na utu. Wakati mwingi hajiamini na ni mwenye hasira za haraka. Herufi I inawakilisha Nyota ya Mshale,
                       HERUFI J
        Mwenye jina linaloanzia na herufi J ni mtu mwenye matamanio,mkweli, mkarimu na muerevu. asiyekubali kushindwa na hupata mafanikio makubwa. Wakati mwingine anakuwa ni mtu mvivu na aliyekosa mwelekeo. Herufi J inawakilisha Nyota ya Mbuzi,
                      HERUFI K
        Mwenye jina linaloanzia na herufi K ni mtu mwenye jeuri. mwenye msimamo thabiti,mashuhuri na mwenye uwezo wa kushawishi na kuamsha hisia za watu wana uwezo wa utambuzi ambao watu wengi hawana. ni mtu asioridhika na hali ya kimaisha. Herufi K inawakilisha Nyota ya Ndoo,
                        HERUFI L
         Mwenye jina linaloanzia na herufi L ni mtu wa vitendo, mwenye hisani na aliyejipanga vizuri kimaisha. Huwa wanapata ajali mara kwa mara. Herufi L inawakilisha Nyota ya Samaki,
                       HERUFI M
        Mwenye jina linaloanzia na herufi M ni mtu mwenye kujiamini sana, mchapakazi na hupata mafanikio. ni mtu mropokaji,mwenye haraka na mwepesi kukasirika. Herufi M inawakilisha Nyota ya Punda
                            HERUFI N
        Mwenye jina linaloanzia na herufi N ni mtu mwenye ubunifu, hisia kali na hupenda kuwasiliana lakini ana wivu sana. Herufi N inawakilisha Nyota ya Ngombe

                             HERUFI O
        Mwenye jina linaloanzia na herufi O ni mtu mwenye subra, mvumilivu na mwenye bidii ya kusoma. Ni mtu mwenye kupenda kutumikia jamii na mwenye uwezo mkubwa wa kudhibiti hisia. Herufi O inawakilisha Nyota ya Mapacha
                         HERUFI P
         Mwenye jina linaloanzia na herufi P ni mtu mwenye uwezo wa kuamrisha na hekima kubwa. Ana nguvu za kiroho lakini anapenda sana kujitumbukiza kwenye mambo ya watu. Herufi P inawakilisha Nyota ya Kaa
                             HERUFI Q
         Mwenye jina linaloanzia na herufi Q ni mtu mwenye kupenda mambo ya asili. Ni watu wasiyoelezeka nawana uwezo wa kuonyesha vitu visivyojulikana hata hivyo ni mtu aliyepooza sana. Herufi Q inawakilisha Nyota ya Simba
                       HERUFI R
         Mwenye jina linaloanzia na herufi R ni mtu mwenye uvumilivu, wenye huruma lakini ana hasira za haraka. Muda wote anakuwa mpenda amani. Herufi R inawakilisha Nyota ya Mashuke
                          HERUFI S
        Mwenye jina linaloanzia na herufi S ni mtu mwenye mvuto mkali wa kuleta utajiri. Ni watu wenye maamuzi ya ghafla na hupenda mageuzi makubwa. Herufi S inawakilisha Nyota ya Mizani
                           HERUFI T
        Mwenye jina linaloanzia na herufi T ni mtu mwenye kupenda ushauri wa kiroho, anatumia nguvu za ziada kusaidia watu na hupata mafanikio baada ya muda mrefu. Ni watu wenye hisia kali sana na ni wepesi kushawishika. Herufi S inawakilisha Nyota ya Nge
                             HERUFI U
        Mwenye jina linaloanzia na herufi U ni mtu mwenye bahati kubwa kwa ujumla. Anapenda uhuru katika mapenzi. Lakini ni mtu mbinafsi, mwenye tamaa na aliyekosa maamuzi. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mshale.
                          HERUFI V
         Mwenye jina linaloanzia na herufi V ni mtu Mchapakazi, wenye bidii na asie choka. Hata hivyo ni watu wasiotabirika. Herufi U inawakilisha Nyota ya Mbuzi.
                         HERUFI W
         Mwenye jina linaloanzia na herufi W ni mtu muwazi, wachangamfuu kupita kiasi na mwenye uwezo wa kutambua mtu mwema na mbaya. Ni watu wenye tamaa na hufanya mambo ya hatari. Herufi W inawakilisha Nyota ya Ndoo.
                          HERUFI X
         Mwenye jina linaloanzia na herufi X ni mtu asiyependa kuwekewa vizuizi katika kwenye anasa na ni rahisi kujiingiza kwenye uzinzi na kujitoa uaminifu. Herufi X inawakilisha Nyota ya Samaki.
                   HERUFI Y (YASINTA)
       Mwenye jina linaloanzia na herufi Y ni mtu mwenye kupenda Uhuru na hawapendi kupingwa jambo lao lolote. Ni watu wanaokosa uamuzi na husababishia kupoteza bahati katika maisha. Herufi Y inawakilisha Nyota ya Punda.
                          HERUFI Z
       Mwenye jina linaloanzia na herufi Z ni mtu mwenye kupenda matumaini na amani. Ni wenye msimamo mkali ila wanashauriwa kufikiria kabla ya kuamua jambo. Herufi Z inawakilisha Nyota ya Ngombe.

Thursday, 16 January 2020

KUSAFISHA NYOTA, MVUTO WA BISHARA KWA KUTUMIA MUOSHA FEDHA



FAHAMU KUHUSU MMEA WA MUOSHA FEDHA

Muosha fedha unaingia kwenye orodha ya mimea saba ambayo inafanya kazi kubwa katika hitaji binaadam. Mti huu huweza kungarisha nyota, kuvuta watu biashara pamoja na mambo mengine.

Miongoni mwa miti saba ambayo inafanana kikazi na muosha fedha ni pamoja na mwita, mfunguo, muharaka miti mitatu naihifadh.

Miti Hii km utaiweka pamoja inaweza kukupa matokeo haraka kwwnye kazi iliyokusudiwa.

Kwa matumizi kwa ajili ya biashara

Tafuta muosha fedha Chumvi ya mawe Pilipili nyekundu unga Mwita

Changanya pamoja choma eneo lako la biashara kwa manuiz asubuhi kabla ya kufungua kwa muda wa ck tatu

Kwa kujifungua na nuksi au mikosi

mambo hayaendi Sawa unalopanga haliwi

Tafuta Kindu 7 Muosha fedha Nazi ya mdondo. Yai la kuku wa kienyeji. majani ya mbaazi unga Mwembe jini

Chukua kindu saba usiku wakati unataka kulala kisha uzifunge fundo moja moja kisha unasema mimi nimefungwa kilakitu na alienifunga simjui sasa namimi nimejiongezea kifungo nafunga njia zangu pia nafunga ufalme wangu na nafunga nyota zangu hadi siku zitakapo fungua hizi kamba. Kisha unaziweka mchagoni unalala na ikifika asubuhi unazitia ndani ya maji kwenyendoo ya kuogea weka na nlvyovtaja hapo juu.

Oga hivyo vyote vikiwa ndani ya hiyo ndoo ya maji kisha unaanza kufungua kindu kwa kusema,

"alie nifunga alijua kamaliza sasa kuanzia sasa najifungua" Ukimaliza kuzifungua uzichome moto halafu nazi na yai ni vya kuvuja kwa manuizi, Unasema wewe yai umefungwa na sijui kama unamtoto wa kike au wa kiume namimi sijui alie nifunga kama ni wa kike au ni wa kiume nitakavyo kufungua wewe yai namimi nifunguke haraka sana, unalivunja. Kisha unakamata nazi unasema wewe nazi hufunga na kufungua namimi najifungua kuanzia sasahivi nafungua nyotayangu, nafungua ufalme wangu, nafungua, nafungua bahati zangu kwa uwezo wa muumba mbingu na ardhi.

Ukimaliza kuvunja zoa katupe jalalan

Kwa ajili ya bahati au mvuto wa mtu
Tafuta muosha fedha unga
Unga wa Misk
Mafuta ya Misk
Mafuta ya alizet

Changanya pamoja Paka na kuchoma kwa manuizi ndani ya ck 7 biidhini llah mambo yako yatafunguka 
Kazi zote muelekee mungu kwanza

Kwa tatizo lolote

+255 745 59 50 89

Whatsapp/Calls

Wednesday, 18 December 2019

HIVI NDIVYO UNAWEZA IFAHAMU NYOTA YAKO KAMA IMEIBIWA AU KUCHAFULIWA

BAADHI YA MAMBO YANAYOWEZA KUASHIRIA KAMA NYOTA YAKO IMEIBIWA AU KUCHAFULIWA

Katika mada yetu ya leo tutaangazia baadhi ya mambo yanayoweza kuashiria kama nyota yako imeibiwa au kuchafuliwa.  Vipo vitu vingi vinavyochangia kuibiwa nyota yako na kupelekea kuharibiwa, kuchafuliwa na kufa kabisa.  Hivyo basi katika kulitambua hilo, tukaona ni vyema tuviorodheshe ili uweze kufahamu na kujtathimini upo katika kundi lipi kati ya haya.

  •  UZINZI : Vitabu vyote vya mafundisho ya imani zote mbili, hapa nazungumzia Uislamu na Ukristo vinatoa onyo kali juu ya mtu mzinzi.  Hii inatupa picha ya kwamba kitendo hiki ni batili na huchangia kuleta uharibifu kwetu sisi wanadamu kama vile maradhi, kuharibu na kuchafua nyota endapo ikatokea mtu uliyezini nae akawa na nuksi mwilini mwake.
  • KUROGWA NA WACHAWI : Silaha kubwa ya adui ili aweze kukushinda ni kufahamu mapungufu au madhaifu yako.  Wanachokifanya wachawi kabla ya kukuroga ni kutazama uimara wa nyota yako na endapo wakapata upenyo wa kuona walau madhaifu madogo basi hutumia mwanya huo kuweza kuharibu nyota yako kisha kukuroga na kukuchezea kadri wawezavyo.
  • KUHARIBIKA KWA MIPANGO YAKO : Kama kuna mipango au mikakati madhubuti uliyojiwekea basi ndugu yangu utashangaa mmoja baada ya mwingine unakufa na kupotea kabisa, hata kama ilitokea uliahidiwa kupata kazi au kupandishwa cheo matarajio hayo huyeyuka na kupotea kama upepo.
  • BIASHARA KUYUMBA : Ikiwa ulikuwa na biashara yako inafanya vizuri kwa kupata wateja na kukuingizia faida, utaanza kuona mabadiliko taratibu ya mtaji kuyumba na duka kufa bila kufahamu hela umepeleka wapi, hata kama kuna watu uliwakopesha mahitaji unaweza kushangaa ukawasahau kabisa hata majina yao.
  • MAHUSIANO KUVUNJIKA : Yaani hapa kila kitu kinakuwa shaghala baghala, unaweza ukamkufuru hata Muumba wako. Kama ulikuwa katika uchumba au ndoa utashtukia imevunjika pasipokuwa zile sababu za msingi zinazopelekea kuvunjika kwa mahusiano mengi kama vile usaliti, wivu au ugomvi.

Haya ni machache tuliyojaliwa kuchambua kwa siku ya leo, 

Pete Za Masonic Immoring Hazina Uhusiano Wowote Na Kuabudu Masheitwaani


Imeandikwa na: Dokta  Maalim Mambikhi Whatsapp/Calls +255 745 59 50 89.
 Maneno yaliyo  zagaa   mitaani  kwamba  eti   watu  wanao vaa  pete za  Masonic  Immoring  ni  waabudu  sheitwani  hayana  ukweli  wowote.

Ikitokea mtu  maarufu  ameonekana  akiwa  amevaa  pete  hizo  basi  moja  kwa  moja  watu  wataanza kumuhusisha  na  habari  za  kuabudu  masheitwani.

Maneno  hayo  ni  uzushi  mtupu  na ambao  hauna  mashiko  yoyote katika  ulimwengu  wa kiroho.

Watu  wanao  eneza  uzushi  huo  ni  watu wenye  ufahamu  mdogo  sana  kuhusu  imani za jadi, imani  za  siri, imani za  kale  na  ulimwengu  usio  onekana  ( ulimwengu   wa  kiroho )  kwa  ujumla.

Pete  za  Masonic  Immoring  ni  pete  ambazo  zimekuwa  zikitumiwa  na  wanadamu  toka  enzi  na  enzi .

Kwa  wewe  ambae  bado  una shikilia  imani kwamba  Masonic  Immoring  ni  pete  za  kisheitwani, nakushauri  ufanye  utafiti  wako  vizuri.

Ukifanya  utafiti  wako  vizuri  utagundua  kwamba  pete  hizi  zilikuwa  zikivaliwa  hadi  na  wafalme  wenye  kuheshimika sana   katika  vitabu  vyote  vitakatifu.

Watu  wanao  dai kwamba  wavaaji  wa  pete  za  Masonic  Immoring  ni  waabudu  shetani, wana toa  hoja  dhaifu  kwamba  watu  wote  wanao  jihusisha  na  uvaaji  wa pete  za  Masonic Immoring  huwa  ni watu  wenye  mafanikio makubwa  sana  katika  maisha  ikilinganishwa  na  watu  wanao  fanya  kitu  kile  kile  kinacho  fanywa  na  watu  wenye  kuvaa pete hizo za  Masonic  Immoring.

 Kwamba  kama  ni  mwanamuziki  basi  anakuwa  juu  sana  kuliko  wana  muziki  wenzake  wanao  fanya  aina  ya  muziki  ule  ule  anao  ufanya  yeye, kama  ni  mfanya  biashara  basi  biashara  yake  inapata  mafanikio  makubwa  sana  kuliko  wafanya  biashara  wenzake  ambao  wanafanya  biashara  kama  ile  ile  anayo  ifanya . Mifano  ipo  mingi  sana.

Hata  hivyo  hoja  hii  ni dhaifu  sana  kwa  sababu  mali  na  mafanikio  vyote  vinatoka  kwa  Mungu  kwa sababu  yeye  ndio  ameumba   Dhahabu, Almasi,Fedha  na vitu  vyote  vinavyo  onekana  na  visivyo  onekana.

Ina  maana  gani  kuwapa  utukufu  masheitwani  kwa  kazi  ambayo imefanywa  na  Mungu mwenyewe. Kwani  ina  maana  Mungu  hawezi  kumfanya  mtu  awe  tajiri au  apate  mafanikio ?

SIRI  YA   PETE   MASONIC  IMMORING  NI  MOJA  TU :  Pete  za  Masonic  Immoring zimetengezwa  kwa  madini  na  vito  vinavyo  kaliwa  na  majini  wazito  wazito, wajini  wakubwa, majini watukufu na  walio  katika daraja za  juu  kabisa katika  ufalme  wa  kijini, majini  wa  kifalme.

Unapo  ivaa  pete  ya Masonic  Immoring unakuwa  umeunganisha  nyota  yako  na  nguvu ya  majini  wanao  kalia madini ,mawe na  vito  vilivyo  tumika  kutengeneza  Masonic  Immoring.

Hivyo  unapokuwa  umevaa  pete  ya  Masonic  Immoring unakuwa  umeingia  katika  agano  rasmi  la  kiroho  la  kuunganisha  nafsi/nyota  yako  na  nguvu  ya  majini  hao kwa  kuwaingiza  majini  hao  katika  mfumo  wa  nyota  yako  na  maisha  yako  kwa  ujumla.

Nyota yako  inaanza  kusafiri  kwa  kufuata  kasi  ya   mkondo  wa  nyota  za  majini  hawa  wa  kifalme kwa  sababu  tayari  nyota  yako  inakuwa  imeunganishwa  na  nyota  ya  majini  hawa na  kuwa  kitu  kimoja.

Katika  hili  la  nyota  yako  kusafiri  katika  mkondo  wa  nyota  ya  majini  hawa  watukufu  mfanano  wake  ni  rahisi  sana.  Yani  ni  kama  vile wewe  kijana  ambae  umezaliwa  na  kukulia  kijijini  kwenye  maisha  ya  tabu halafu  ghafla  ukapata  bahati  ya  kuajiriwa  na  mwanamuziki  mkubwa  anae  safari  sana  katika  nchi  mbalimbali  duniani .

Nchi  ambazo  hujawahi  kuota  kufika.  Utaanza  kusafiri  na  mwanamuziki huyo  katika  nchi  hizo.

 Kilicho  fanya  wewe  ufike  katika  nchi  hizo  ni  nyota  ya  mwanamuziki  huyo.

 Kwamba  kwa  sababu  yeye  ni  mwanamuziki mkubwa  na  anae  pata  mialiko  ya  kutumbuiza  kwenye  nchi  mbalimbali,  na  kwa  sababu  wewe  labda  umepata  kazi  ya  kuwa  mpiga  picha  wake, au  mwandishi  wake, basi  utakuwa na  wewe  unasafiri  katika  nchi  hizo  na  mwanamuziki  huyo.

Kwa  lugha  nyingine  utakuwa  una  safiria  nyota  ya  mwanamuziki  huyo.

Vivyo    kuhusu  pete  ya  Masonic  Immoring. Unapo  vaa  pete  ya  Masonic  Immoring  basi  unaanza  kusafiria  nyota  ya  majini  wanaokaa  kwenye  madini, mawe  na  vito  vilivyo  tumika  kutengeneza  Immo  Ring.

Kiuhalisia kabisa  wewe hukustahili  kusafiri  katika  nchi  hizo  lakini  umestahilishishwa  kwa  sababu  ya  agano  lako  na  mtu  anae  stahili kusafiri  katika  nchi  hizo.

Majini  hawa  wana  sifa  moja  kuu, kwanza  huwa  hawakai  na  kitu  chochote  kichafu  kama  majini  wa  baharini, kwa  hiyo  kama  utakuwa  na  kitu  chochote  kichafu  ndani  ya  mwili  wako,uwe  umetupiwa  uchawi,  majini /mapepo wachafu/mizimu mibaya, kijicho  au  kifungo  chochote  kile  cha  kichawi ndani  ya  mwili  wako, vitu  vyote  hivyo  vitafukuzwa  ndani  ya  mwili  wako  kwa  sababu  majini  wanao  kaa  kwenye  vito,madini na mawe  yaliyo tumika  kutengeneza  Masonic  Immoring   huwa  hawakai  na  kitu  kichafu.

Majini  hawa  watafukuza  shari zote  ndani  ya  mwili  wako  na kuvuta  heri  zote katika  maisha  yako  sambamba  na  kuzuia  shari yoyote  ile iliyo elekezwa  kuja  kwenye  mwili  wako.

Majini  wanao  kaa ndani  ya  vito na  madini  yaliyo  tumika  kutengeneza  Masonic  Immoring hawapendi  uchafu  na  hawakai  na  vitu  vichafu.

Ndio  maana  basi  mtu  anae  vaa  pete  hii, huwa  haruhusiwi  kunywa  pombe  huku  pete  ikiwa  kidoleni,  au  pombe  ikiwa  mwilini.

Haruhusiwi  kufanya  zinaa  huku  akiwa  ameivaa  pete  hii  tukufu  na  haruhusiwi  kujisafisha   baada  ya  kumaliza  haja  kubwa   huku  pete  ikiwa  kidoleni  kwa  sababu  pete  hii  huvaliwa  mkono  wa  kushoto.

Ilhali  mwanamke  haruhusiwi  kuvaa  pete  hii  akiwa  kwenye  siku zake.

Na  mtu yoyote  Yule  awe  mwanamke  au  mwanaume  baada  ya  jimai  anatakiwa  kukoga  kwanza  kabla  ya  kuivaa  tena  pete  hii.

Pete  zote  za  Immoring  zina alama  kama  inavyo  onekana  hapo  juu, kwa  hiyo kwa  mtu  yoyote  Yule  atakae  hitaji  pete  ya  Masonic Immoring , kitu  cha  kwanza  anacho  takiwa  kukitazama  ni  alama ya  pete  hiyo  kama inavyo  onekana  pichani.

Na  kama  unahitaji  pete  ya  Masonic  Immoring, basi  wasiliana  nami  

Sunday, 15 December 2019

DAWA YA KUPANDISHA NYOTA NA KUIFANYA NYOTA YAKO

DAWA YA KUPANDISHA NYOTA NA KUIFANYA NYOTA YAKO

*DAWA YA KUPANDISHA NYOTA NA KUIFANYA NYOTA YAKO KUNG'AA*

Dawa Hii Kama Wewe Ni Mfanyabiashara Itakufanya Ung'ae Na Uvutie Katika Biashara Yako Hali Ambayo Itakufanya Kuwavuta Pamoja Na Kuongeza Idadi Ya Wateja Katika Biashara Yako.

Dawa Hii Kama Wewe Ni Muajiriwa Utapendwa Na Wafanyakazi Wenzako Na Bosi Wako Atakupenda Kulingana Na Utakavyonuia

Dawa Hii Kama Watu Wanakudharau Hawakuheshimu Wanakuchukia Bila Sababu Now Time Ni Zamu Yako Kung'aa Na Wewe Lazima Ukubalike

Dawa Hii Kama Unawasiwasi Sana Na Mashaka Woga Bila Sababu Utakuwa Unajiamini mbele za watu baada ya kujipaka na mchanganyiko dawa hizi
*Wasiliana na Maalim Dr Mambikhi WhatsApp/Calls +255 745 59 50 89*

Wednesday, 11 December 2019

KUONDOA NUKS,MIKOSI,KIZA CHA MIAKA NA MIAKA,MVUTO WA BIASHARA NA NDOA

  Talasimu Hii πŸ‘†πŸ‘† kaz zake kama kichwa cha habali kinavyo sema kuwa dua Hii inafunga vifungo ,mikosi,mabalaa,na pia inaondosha maradhi ya amina yoyote Yale kwenye mwili or pahala Fulani .
Kama unaitaji mvuto basi chola talasimu Hii kwanza kisha tumia kuoga kwa mtindo wa kujipakaa kwa muda wa siku 7 kisha ndio utengeneze talasimu za mivuto wapo watu wanalalamika baadhi yao eti kwamba wametumia matalasimu yangu lakin hawakufanikiwa na wengine walio wengi alhamdulila wanaleta mrejesho kwa WhatsApp na kwenye call za kawaida wanapiga wanatuma SMS +255 745 59 50 89 ,
Hata kama wew ni tabibu jua wew kila siku unapigwa vita basi uwe mwingi wa kuoga madawa ya hapa na pale ya kujiagua na zohari maana ukimtoa nuks mgonjwa lazima zitabaki kwako chembe chembe je ukiwatibia zaidi ya 9 unazani kwenye mwili wako hujakuwa jalala sasa basi nyie musio fanikiwa na talasimu zangu fata nyiradi hizi kwanza unatakiwa uwandae talasimu hii kama nilivyo sema apo awali ....
     Chola talasimu hii kwa wino mwekundu wa zafarani kisha uwizungushie Surat Alan nashrah X3 unakomea panapo sema fainama al usil yusira.
    Kisha talasimu hiyo utaisomea Surat yasini X3 .matumizi ni kunywa na kuoga siku7,dua hii inatoa kila kitu kwenye mwili wako ambacho kichafu kuanzia jini mahaba mikuli visiki mahembe nuksi za kila rangi hii inaondoa ni mujarabu sana na maradhi yoyote Yale mwilini pia vile vile ukimaliza kuitumia hivyo iyandae tena kama apo awali kisha itundike kwenye biashara yako na kama wew unataka kuolewa Kuowa basi tumia kuoga kwa mtindo wa kujipakaa hakikisha usipakie sehemu chafu maana utapata madhara makubwa (chunga hili pindi unavyo jisafisha wew na usafishe na biashara yako kama 

 kwenye fremu basi angalia kumwaga mwaga kudekia kila siku X1 mpaka siku 7 ndio kisha uweke talasimu yako juu ya mlango wako na kama wew machinga basi mwaga mwaga na maji kwenye vitu vyako kwa jujuu yani kisha talasimu itengeneze kama kiamuret or azima kuwa nayo unapo tumia pesa hii ni hatali sana kwa mvuto).

Kwa mafunzo tiba na ushauri Wa magonjwa Kwa tiba asili. Je unasumbuliwa na ndoa yako, biashara inaandamwa na chuma ulete, unasumbuliwa na wachawi kwenye mji wako? Husiteseke tena ingia hapa
https://chat.whatsapp.com/Jcn23l8qSNgJaoRk7uZMpB

Friday, 4 October 2019

WhatsApp Group

Wasumbuka na maisha? Je kila unalolifanya halikubaliki kwenye jamii au kazini kwako? Unasumbuliwa na mmeo au mkeo?
Biashara inaandamwa na chumaulete? Husipate tabu tena ingia kwenye ukurasa wa WhatsApp wa Maalim Dr Mambikhi ili kujifunza tiba na utatuzi Wa shida mbalimbali.
Bofya link kujiunga 
https://chat.whatsapp.com/Jcn23l8qSNgJaoRk7uZMpB

Saturday, 28 September 2019

JINI MAHABA NI NINI?

Jini mahaba ni jini {pepo,shetani} yeyote alie muingia mwanaadamu kwa lengo la kufanya nae uchafu wa zinaa.

VIPI ANAWEZA KUMUINGIA MTU?

 Jini mahaba huwaingia watu kwa sababu nyingi miongoni mwazo ni

kulala bila ya nguo au nguo nyepesi sana bila ya kusoma dua hasa nyakati za joto

2.wakati wa kufanya tendo la ndoa na wanandoa kusahau kusoma dua wakati wa tendo{na hapa ndipo huwaingia watu zaidi}

3.kujitazama ktk kioo kwa muda mrefu bila ya kusoma dua na hasa kwa wanaopenda kujitazama wakiwa uchi

4.kuogelea ukiwa uchi katika vyanzo vya majibila ya dua {hii hupelekea kuingiwa hasa na majini aina ya ghawwaas]

5.kutupiwa na wachawi{mchawi huweza kumuita shetani kichawi na akafanya nae makubaliano na kufunga mkataba kisha akatumwa shetani akuingie }

6. kuingia chooni bila dua {vyooni kuna majini aina na khubuth na khabaaith hivyo anaeingia bila ya dua anaweza kukumbwa na majini hawa na watu wengi wanaoanguka chooni huwa ni kwa kuangushwa na aina hii ya majini}

DALILI ZAKE

majini mahaba huwa na dalili nyingi na hutofautiana kutegemeana na aina ya jini alie kuingia

1. ndoto za kufanya jimai mara kwa mara hasa na mtu unae muheshimu km kaka dada mama baba nk {si kila ndoto ya kufanya mapenzi ni dalili ya jini wakati mwingine ndoto ya kuota unafanya jimai hadi kufikia mshindo hutafsiriwa kama kupata wepesi na mafanikio katika mambo ya muotaji

2. kuharibika ujauzito bila sababu za kidaktari

3. kuchukia tendo la ndoa kuoa au kuolewa na hata kumchukia mwenza wako akiwa karibu nawe na hujihisi kumpenda sana akiwa mbali

4.ndoto za kuota unazaa kunyonyesha au kulea mtoto

5. mwanamama kuvurugikiwa siku za hedhi

6.maumivu makali chini ya kitovu wakati wa tendo la ndoa au hedhi[hili husababishwa pia na vitu mbali mbali km mgoro na baadhi ya bakteria wanao shambulia viungo vya uzazi

7. kutosikia hamu ya tendo la ndoa bila sababu za kidaktari

8. ujauzito kutoweka baadhi ya nyakati na mjamzito kuhisi km hana kabisa ujauzito

9. kupenda sana maasi na kuchukia dhikri na ibada

10. mipango kuharibika bila sababu za msingi

11. kutokuwa na nguvu za kijinsia bila sababu za kidaktari

12. kujihisi umeonewa hadi unafikia kulia bila sababu

13. moyo kwenda mbio bila sababu za kidaktari

14. kifua kuwa kizito km umebeba mzigo au kichwa

15.kuota ndoto za kweli wakati sio mchamungu

16.ndoto za kukimbizwa na wanyama wakali km simba nyoka chui nk

17.kupiga kelele bila sababu na unashindwa kujizuia

hizi ni baadhi tu ya dalili zipo nyingi sana

MADHARA YAKE

jini huyu anapomuingia mwanadamu huweza kumpatia madhara yafuatayo

1.kuchukia kuoa au kuolewa

2.kuchukia watu wa jinsia tofauti

3. kutopata mtoto

4. kuvurugikiwa mambo yake bila sababu za msingi

5. gundu [an kis]

6.kuchukiwa bila sababu n.k

TIBA YAKE

Chukua dawa zifuatazo

1. manemane mruturutu kiberiti upele na karafuu maiti changanya ujazo sawa atumie kujifukiza asubuhi na jioni

2. chukua mafuta ya mkunazi zaituni habatisaudaa, ndimu na kitunguu swaumu ujazo sawa ila zaituni yatakiwa kuwa marambili ya ujazo wa mafuta mengine weka miski ya unga kijiko kimoja cha chakula tumia kujipaka asubuhi na muda wa kulala kwa muda wa wiki tatu mfululizo

Kwa ushauri na dawa za magonjwa mbalimbali wasiliana nami Maalim Mambikhi bingwa Wa tiba asili

+255 745 59 50 89

Tuesday, 3 September 2019

POWERFUL OIL(Mafuta ya Maajabu)

1.POWERFUL OIL
HAYA MAFUTA YANATIBU:
KUONDOA NGUVU ZA GIZA
KUSADIA KUFA GANZI KATIKA BAADHI YA VIUNGO, MIGUU KUWAKA MOTO
KUFUKUZA MAJINI NDANI YA MWILI
KUZUIA KUOTA NDOTO ZA KUTISHA
KUOTA UNAINGILIWA KIMAPENZI USIKU
KUZUIA WACHAWI KUINGIA NDANI YA NYUMBA YAKO KWA NGUVU ZA GIZA( JIPAKE KABLA YA KULALA MWILI MZIMA KIDOGO TU NA NYUNYUZIA KWENYE NYUMBA YAKO KILA BAADA YA MWEZI HASA KWENYE PEMBE , MADIRISHA NA MILANGONI)
KUONDOA HALI YAKUWA NA WASIWASI NA KUKATA TAMAA NA HALI YA KUCHANGAMKA(JIPAKE USONI NA KICHWANI NA KIFUANI NA UTAJISIKIA UNAKUWA NA HALI MPYA NA KUONGEZA NGUVU YA KUTOKATA TAMAA)
Wasiliana na Maalim Dr Mambikhi Kwa simu no +255 745 59 50 89

Saturday, 6 July 2019

JINSI  YA  KUMZINDUA  MWANAUME  ALIYE  LISHWA  LIMBWATA  LA  KUSINI

Angalia Video Hapa chini kwenye linkπŸ‘‡πŸ‘‡
LIMBWATA LA KUSINI

JINSI  YA  KUMZINDUA  MWANAUME  ALIYE  LISHWA  LIMBWATA  LA  KUSINI
 Uchawi  wa  mapenzi  kutoka  kusini  mwa Tanzania  ndio  uchawi  wa  mapenzi  wenye nguvu  kuliko  uchawi  mwingine  wowote  ule wa  mapenzi  ambao  umewahi  kuusikia.  Mume  wako, kaka  ako  au  baba  ako  akilishwa  limbwata  la  kusini  basi  hapo  wewe  hesabu  maumivu  kwa  sababu  uchawi  huu  ni  hatari  sana.  Tofauti  na  uchawi mwingine  wa  mapenzi, limbwata  la  kusini  ni SUMU YA  KICHAWI  AMBAYO  INAENDA  KUUA UBONGO  WA  MTU  ALIYE  LISHWA  NA KUMFANYA  AFANYE  KILA  KITU  AMBACHO  MLISHAJI  ANAKITAKA.
Nikiwa  kama  Tabibu  wa  Jadi  nimekutana  na  kesi  nyingi  sana  za  watu  walio  lishwa  limbwata  la  kusini. Pamoja  na  kwamba wanaume  ndio  wahanga  wakuu  wa  uchawi huu  yani  wanaume  ndio  wanao  ongoza  kwa  kulishwa  uchawi  huu  hatari na  mbaya  kabisa  kuwahi  kutokea  katika  historia  ya  uso  wa  dunia  lakini pia  wanawake  pia  hulishwa.  Siku  hizi  maisha  yamebadilika  sana  kwani  hata  wanaume  nao  wanatembelea  vilingeni kutafuta  uchawi  wa  mapenzi.
Watu  wengi w anao  lishwa  uchawi  huu  huwa  wana  haribikiwa  na  kufilisika  kabisa  kwa  sababu  lengo  la  mlishaji  huwa ni  kupata  fedha  na  mali  kutoka  kwa  mlishwaji.
Katika  lugha  ya  kitabibu  uchawi  huu  huwa  unajulikana  kama  “ TEKO “  kwa  sababu  mtu  aliye  lishwa  uchawi  huu  anakuwa  kama  mtu  aliye  tekwa  na mtu mwenye  silaha  nzito  mfano  bunduki. Mtu  akitekwa  kwa  bunduki ile  bunduki  inakuwa  sio  bunduki  tena  bali  inakuwa “ Remote  Control”  ambayo  kazi  yake ni  kumcontrol  mtekwaji  na  kumuamuru  kufanya  anacho  kitaka.
Mtu  aliye  lishwa  uchawi  huu hufanya  kila kitu  anacho  amriwa  kufanya  na  mtekaji.
Uchawi  huu  umeharibu  maisha  ya  watu wengi  sana.  Familia  nyingi  zime  vunjika  kwa  sababu  ya  uchawi.  Watoto wengi  wametelekezwa na  kuharibikiwa  maisha  kwa  sababu  ya  uchawi  huu.  Kibaya zaidi  wahanga  wa  uchawi  huu  wanazidi  kuongezeka  siku  hata  siku. Nimekuwa  nikipokea  ujumbe kutoka  kwa  watu  wengi  wakiniomba  nitoe somo kuhusu  namna  ya  kujikinga  dhidi  ya uchawi  huu pamoja  na  kuwazindua  watu  ambao  tayari  wamelishwa  uchawi  huu.
Nimeandaa  makala  maalumu  kupitia  blogu yangu hii ambayo  inaelezea A  TO  Z  kuhusu  uchawi  huu, na  jinsi  ya kujikinga  nao  au  jinsi  ya  kumzindua  mtu  alie lishwa  uchawi  huo.
Kila  nikipata  nafasi  nitakuwa  naweka hapa maelezo  kuhusu  namna  ya  kujikinga  na  kukabiliana  na  uchawi  huu.
Zipo  njia  nyingi  sana  ambazo  wanazitumia wacahwi  kutengeneza  uchawi  huu  hatari  wa mapenzi. Nitakuwa  naeleza  njia  moja  wapo  baada  ya  nyingine  na  namna  ya  kumzindua mtu  aliye  lishwa  uchawi  kwa  njia  husika.
Kwa  kuanza  leo  hapa  nitaeleza  kwa  ufupi  njia  moja  wapo  wanayo  tumia  wachawi:
Kwa  kuanza  wachawi  hufanya  vitu  vifuatavyo :

1.       Huchukuliwa  mzizi  ulio okotwa  kwenye mwanandani  wa kaburi ( Mwanandani  wa  kaburi  ni  kishimo  cha  ndani  ya  kaburi. Sasa  watu wakiwa  wanachimba  kaburi  halafu  kwenye  mwanandani  wakikuta  kuna  mzizi  humo  wanachukua  kipande  cha  huo  mzizi. Huo mzizi  sasa  ndio  unao  enda  kuingia kwenye  pishi  la  hilo  limbwata  la  kusini  la  aina  ya  kwanza  ambayo  ninaielezea hapa )
2.       Anachukuliwa  mdudu  anaeitwa  Nyunga. Huyu  nyunga  ni  mdudu  wa  porini  ambae  anafanana  sana  na  panya na  ana  sifa  moja  ya kipekee. Yeye  akivuka  tu njia  anakufa.
3.       Linachukuliwa  tawi  la  mti  mmoja  wa  porini. Huu mti  una  sifa  moja  ya  kipekee  sana. Kila  ndege  anae  tua  juu  ya  mti  huo  anakufa, kasoro  ndege  mmoja  tu  ambae  anaitwa “ Nditi “
4.       Udongo  wa  kichuguu  bubu
5.       Udongo  wa kwenye  njia  panda  jike (  NJIA  PANDA  JIKE  NI  NJIA  PANDA  AMBAYO  ZIMEKUTANA  NJIA  NNE  NA  NJIA  PANDA DUME  NI  NJIA  AMBAYO ZIMEKUTANA  NJIA TATU )
6.        Yanachukuliwa matawi  na  mizizi  ya miti  miwili  iliyo  sehemu moja  lakini mti mmoja  mrefu  na  mwingine  mfupi, yani mti mmoja unauzidi  mti mwingine  urefu.  Huo mti  mrefu vinafungwa  vitu  vya  mwilini  vya  mtu  anae  taka  kumlisha  mwenzake  limbwata  hili  la  kusini  na  mti  mfupi  vinafungwa  vitu vya mwilini  vya  mtu ambae  amekusudiwa  kulishwa  huo  uchawi.
7.       Aina  ya  panzi  wasio na  mabawa. Hawa panzi  hawaruki  kwenda  mbali. Panzi hawa  huchukuliwa na  kusagwa . ( Hawa  ni  tofauti  na  wale panzi  wajulikanao  kama  gugwa ambao  hutumiwa na  wachawi  kumvuta na  kumuita  mtu  aliye  mbali aje  haraka  sana )
8.       Mjusi  wa  ndani ya  nyumba
9.       Maji  ya  Tunge (  Haya  ni  maji ya  kichawi ambayo  hutumiwa  na  wachawi  kuwalisha  watu matunge  wasahau  kuhusu  maisha  yao  yaliyo  pita )
10.   Nyama  ya  n’gombe  na  paka. Hii  nyama  ya  n’gombe  hupasuliwa  na  kuwekwa  dawa  iliyo  changanywa  na  talasimu.  Halafu nyama  hiyo huandikwa  talasimu  la  kichawi  kwa  kutumia zaafarani  nyekundu  na  miski. Hii  hutumika kumlisha  paka.” Kanyama  ka  paka “ lengo  ni  kumfanya  mwanaume  anae lishwa  uchawi huu  amn’gan’ganie  mlishaji  kama  paka  am’ganganiavyo  mtu  anaekula  nyama  hata akifukuzwa  vipi.
11.    Kichwa  cha  kondoo  au  kondoo  mzima  mzima  analishwa  dawa , talasimu  na  vitu  vya  m,tu  aliekusudiwa   kufanyiwa  uchawi na kisha  kwenda  kuzikwa  kaburini.
Pamoja  nma  vitu  vingi sana  ambao  muda hauniruhusu  kuvielezea  vyote  leo.  Vitu  hivi vinatumika  kutengeneza  hilo  TEKO  ama  LIMBWATA  LA  KUSINI  kwa ajili  ya  kumroga  mwanaume  aliye  kusudiwa . ( Kumbuka  hii  ni  aina  moja  tu )
Uchawi  huu  ni  mbaya  sana.  Mwanaume aliyelishwa  uchawi  huu  kama  alikuwa  na  mke  na  watoto  basi  wote  atawasahau.  Yani  anakuwa  kama  hajawahi  kabisa  kuwa  na  familia. Ni uchawi  hatari  sana  na  umevunja familia  za  watu  wengi  sana.
Kesho  nitaendelea  na  aina  nyingine  ya  TEKO  ( LIMBWATA  LA  KUSINI )  na  nitamalizia  kwa kuelezea  njia  gani  unazo  weza  kuzifanya wewe  mwenyewe  ili  uweze  kujikinga  na kujiepusha  na  kurogwa  uchawi  wa  aina  hii  pamoja  na  kumzindua  mtu  aliye rogwa uchawi  huu )
Kwa  makala  zangu  nyingine,
Wasiliana na maalim Dr Mambikhi Whatsapp/Calls 255 745 59 50 89

Asalaam aleykum wanagloup leo nawaletea dawa adimu na adhwimu bado nipo safalini nimekuja kuchimba madawa ya tiba huku nimekutana namtihuu unaitwa mdocteri nimti hatali ndomana nimeonelea niwaletee somohili. litwaalo maajabu ya. Mdocteri cjui niseme dhahabu au almasi mdocteri ni nidawa ilikuwa inatumika na waganga wa zamani wakongomani. na walundi pamoja na wa nigelia mtihuu waliutumia sana hasa katika mambo ya mazingaombwe mvuto na kufunguwa ndoto. Na kubashili mambo mbalimbali na kun'golea vitu vibaya vilivyofukiwa aldhini umeitwa mdokteri. Mtihuu. Pia unanguvusana kwaupande wanjozi loho wamtihuu au malaika wa mtihuu ndio wenyenguvu za kujuwa na kutambuwa kutabili kubashili ipasavyo mwenyezimungu kaumba mitiii lakini kusemakweli mtihuu kaupendeleasana mti huu kunabaadhi ya waganga wa zamani walikuwa wanauweka kwenye msinga ili kuweza kupata nguvu za kiloho za kutabilia. Na kupimia watu na kufanyia kazi mbalimbali nakumbuka babuyangu mzee kiboko og. alikuwa na msinga wake alikuwa anautuma popote unaenda na unaludi wenyewe bilatabu huo ndio uganga wa zamani bhana wenzetu walikuwa hawabaatishi sio ckuhizi watu wanaenda kuusomea uganga au wengine wamesoma madlasat kaifadhi duwaa mbilitatu bac nayeye mganga tena anatamba mkikolofishana kidogo utamsikia wewe unanijuwa vizulimimi waulizewenzio nawanakibuli yaani utadhani makhudam wooote duniani wapokwake namatapeli wamekuwa wengi adi wameufanya uganga umeshuka hadhi soote twaonekana wezi2 tunaendelea. Mdocteri hutumika pia kwenye maswaala ya kuondowa mapepo katika mwili wa mtu na hutumika katika maswaala ya kuvuta njozi maana uganga bila njozi wewe siomganga pia mdocteri pia hutumika katika kutengenezea chumaulete pia hutumika kutowa nux vifungo na kuongeza mvuto kwenye biashala ambapo utauchanganya mdocteri pamoja na mvumbasi dikulu utamwaga kwenye kazizako au biasharayako na kilakitu kitafunguka na kitaenda Sawa sawia pia unaweza kujitngenezea nguvu za ziada kupigia mtihuu pia unaweza kujijengea jicho la tatu ukawa na uwezo kuona vilivyo fichikana yaaan huumti nikiboko.

MITI TIBA


Saturday, 20 October 2018

IJUE NYOTA YAKO

IJUE NYOTAYAKO

NYOTA

JINSI YA KUFAHAMU NYOTA YAKO CHUKUA JINA LA BABA YAKO CHUKUA JINA LAKO  NA LA MAMA GAWANYA  KWA KUMI NA MBILI.

1.           IKIBAKI MOJA NI PUNDA.

2.           IKIBAKI MBILI NI NG,OMBE.

3.           IKIBAKI TATU NI MAPACHA.

4.           IKIBAKI NNE NI KAA.

5.           IKIBAKI TANO NI SIMBA.

6.           IKIBAKI SITA NI MASHUKE .

7.           IKIBAKI SABA NI MIZANI .

8.           IKIBAKI NANE NI NGE.

9.           IKIBAKI TISA NI MSHALE.

10.      IKIBAKI KUMI NI MBUZI.

11.      IKIBAKI KUMI NA  MOJA NI NDOO.

12.      IKIBAKI KUMI NA MBILI NI SAMAKI.

NA PIA KUNA NYOTA ZA AINA NNE AMBAZO NDIZO NYOTA ZA ASILI NA UKITAKA KUZIJUA NYOTA HIZO UNACHUKUA JINA LAKO LA BABA NA LA MAMA UNAGAWANYA KWA NNE

1.           IKIBAKI MOJA NI  MOTO .

2.           IKIBAKI MBILI NI UDONGO.

3.           IKIBAKI TATU NI UPEPO.

4.           IKIBAKI NNE NI MAJI.

NYOTA HIZI NDIZONYOTA ZA ASILI AMBAZO INATAKIWA TUZIFAHAMU MFANO MTU MWENYE NYOTA YA MOTO HATAKIWI KUFANYA KAZI ZA MTU MWENYE NYOTA YA MAJI MAANA NYOTA YAKE ITAZIMIKA.

MWENYE NYOTA YA MOTO KAZI ZAKE NI UDREVA,UASKARI,UMACHINGA,HOTELI,, BIASHARA, ZINAZOHUSIKANA NA KUSAFIRI SAFIRI AU SALUNI MAANA SALUNI MOTO UNATUMIA UMEME ,FUNDI WELDING,NA KAZI ZINAZOHUSU UPEPO MAANA MOTO NA UPEPO ZIKO PAMOJA.

NA PIA NYOTA YA MAJI NA UDONGO ZINAFANYA KAZI MOJA.KAZI ZAO NI UVUVI,KULIMA ,UFUGAJI,KUCHIMBA MADINI, FUNDI WASH,FUNDI UJENZI.N.K.

MTU MWENYE NYOTA YA MOTO INATAKIWA AOLEWE NA MTU MWENYE NYOTA YA UPEPO.

NA MTU MWENYE NYOTA YA MAJI INATAKIWA AOANE NA NA MTU MWENYE NYOTA YA UDONGO.

WATU WENGI NDOA ZAO HUHARIBIKA MAANA HAWAFATI MAMBO HAYA .KUJUA  NYOTA NI MUHIMU SANA NA HATA KIBIASHARA INATAKIWA TUJUE NI HERUFI GANI ZA KUANDIKA KATIKA BIASHARA AU KATIKA MADUKA YETU.

`

PIA KUNA KUZIJUA NYOTA KWA KUTUMIA HERUFI MFANO MWENYE HERUFI INAYOANZA NA   A,=PUNDA. B=NG,OMBE.   C=MAPACHA.    D= KAA.   E= SIMBA.     F=MASHUKE.   G=MIZANI .  H=NGE.      I=MSHALE.   J==MBUZI.  K= NDOO.  L=SAMAKI.  M=PUNDA. N=NG,OMBE.  O=MAPACHA. P=KAA.   Q=SIMBA.  R=MASHUKE.   S=MIZANI.     T=NGE.  U=SAMAKI.   V=MBUZI.    W=NDOO.  X=SAMAKI.    Y=PUNDA.   Z=NG,OMBE..NA HIZO NI KUZIJUA NYOTA KWA KUTUMIA HERUFI YA MWANZO WA JINA LAKO.

PIA KUNA KUZIJUA NYOTA KWA KUZALIWA  KUTOKANA NA MWEZI ULIOZALIWA MFANO.

TAREHE 19   MWEZI  WA   1   HADI  TAREHE   20  MWEZI    WA    2  NI  NDOO.

TAREHE 21   MWEZI  WA   2   HADI  TAREHE   20  MWEZI    WA      3  N I  SAMAKI.

TAREHE 21   MWEZI   WA    3   HADI  TAREHE   20  MWEZI   WA     4   NI   PUNDA.

TAREHE 21   MWEZI  WA   4    HADI   TAREHE   20    MWEZI  WA     5     NI NG,OMBE.

TAREHE 21 MWEZI  WA    5       HADI   TAREHE  20   MWEZ I WA     6    NI MAPACHA.

TAREHE 21 MWEZI WA    6        HADI  TAREHE   20     MWEZI  WA    7    NI KAA.

TAREHE 21 MWEZI WA    7       HADI   TAREHE    21       MWEZI  WA  8     NI  SIMBA.

TAREHE 22 MWEZI WA   8       HADI   TAREHE     22 MWEZI      WA      9        NI  MASHUKE.

TAREHE 23  MWEZI WA 9      HADI     TAREHE       22 MWEZI    WA     10    NI  MIZANI.

TAREHE 23 MWEZI WA 10     HADI     TAREHE    21 MWEZI     WA       11    NI     NGE.

TAREHE 22 MWEZI WA 11 HADI TAREHE 21 MWEZI   WA  12  NI   MSHALE.

TAREHE 21 MWEZI WA 12 HADI TAREHE 18 MWEZI WA  KWANZA  NI MBUZI.

HIZO NDIZO  NYOTA KWA NJIA YA TAREHE .

PIA NYOTA HIZI ZIKO KATIKA MAGURUDUMU KAMA NILIYOYATAJA HAPO NYUMA MFANO.

1.           NDOO=     MOTO

2.           PUNDA = MOTO.

3.           NG,OMBE =UDONGO

4.           MAPACHA = UPEPO.

5.           KAA=MAJI.

6.           SIMBA=MOTO.

7.           MASHUKE= UDONGO.

8.           MIZANI =UPEPO.

9.           NGE=MOTO.

10.      MSHALE=MOTO.

11.      MBUZI =UDONGO.

12.      SAMAKI = MAJI.
Kwa mawasiliano +255 745 59 50 89

Wednesday, 22 August 2018

NUKSI NI NINI


#-NUKSI-Ni neno la kiarabu ambalo lina maana ya machafuko ,maangamiko,maharibiko. Ambalo kwa kiswahili tuna liita neno hili ni mkosi ambayo ndio maana halisi na sambamba ya msamiati huo.

#NUKSI- ni hali inayo mkumba mtu na kumfanya kuwa na dhiki na ugumu katika kuyaendeka mambo yake na kupata kile anacho kihitaji kwa nafasi yake.

#Tunapo zungu mzia nuksi tuna zungumzia ujumla wa muambatano na visababisha vya ukwamaji wa mambo kwa watu mbali mbali.


#Nuksi kwa ujumla wake zimegawanyika katika aina nyingi ambazo kila moja na sababu zake ambazo hupelekea mtu kuingia katika matatizo kwa uzito wa nuksi yake.
    
   VISABABISHI VYA NUKSI/MKOSI.

A)-#Kukumbwa na kafara za watu manjiani.

B)-#Nuksi ya kuambukizwa na mke/mume.

C)-#Nuksi ya kuletwa na majini.


D)-#Nuksi ya masononeko ya wazazi.

E)-#Nuksi ya kufungwa na asili ya ukoo wa mtu.

F)-#Nuksi ya laana za wazazi/kiapo.

G)-#Nuksi ya kufanyiwa uchawi.

Vyote hivi ni baadhi ya miongoni mwa vitu ambavyo huweza kusabaisha nuksi/mkosi kwa binaadamu.

#Watu wengi wamekuwa wakisumbuka na Mikosi/nuksi pasi na kujua pia ni Nuksi gani inayo wasumbua.

Hapa leo tunazunhumzia aina  moja ya nuksi/mkosi.

1-#Nuksi ya kuikumba -hii ni nuksi ambayo mtu anaikumba yaani hakukusudiwa kufanyiwa kitu kibaya na wachawi wala adui wake.

Hii hutokea pale mtu anapo pita sehemu ambayo kuna watu walifanya kafara ya kutoa nuksi ama kujifungua kutokana na matatizo aliyo nayo.

Endapo mtu atakatiza katika eneo hilo akiwa ni wa mwanzo ni tangu kafara hiyo kufanyika basi mtu huyo ana weza kuipata niksi hiyo.

Nuksi hiyo ambayo huanza kujitokeza matokeza kwake kuanzia siku moja kwa ukamilifu wake ama siku ya nane yake tangu kumkumba nuksi hiyo.

#Mtu huyo anaweza pia kuanza na kupata homa kama kafara hiyo ilikuwa kubwa na hato pata homa endapo kafara hiyo haiku chinjiwa mnyama wala hakikuchomwa kitu miongoni mwaka vitu vya kafara hiyo.

DALILI ZA MTU MWENYE NUKSI/MKOSI.

1-#kuchukiwa kwa sababu za kawaida zisizo na maana.

2-#kukwama mambo yote ghafla.

3-#kushindwa kujisaidia mwenyewe.

4-#kujihisi una mapungufu wewe Mwenyewe na kujiona kama una kasoro.

5-#kuachwa na mpenzi ghafla.

6-#kusimamishwa kazi pasi na sababu ilio nyooka.

7-#kufa kwa mawasiliano na watu wako wa karibu.

8-#watu kuku sahau kwenye mahala pa kufanya kipato.

9-#kukosa msaada kwa mwenye uwezo wa kukusaidia.

Kwa Tiba na ushauri
+255 745 59 50 89
Website : sales@drmambikhi.com
E mail: mambikhitibaasilia@gmail.com